BIG 4 MILL

big4mill.blogspot.com.

Usisite kutembelea blog yako

Karibu nawe mahali popote... - big4mill.blogspot.com.

Tunaishi pamoja wakati wowote

http://www.big4mill.blogspot.com for more info - big4mill.blogspot.com.

Kazi zetu ni...

Tunaelimisha, kuburudisha na kadhalka.

Pata habari mbalimbali

Ndani na nje ya Tanzania/ kitaifa na Kimataifa - big4mill.blogspot.com.

Friday 30 August 2013

TUMERUDI

Thursday 15 August 2013

respect 2 sauty byego

Tuesday 6 August 2013

AUDIOS - PNC HARUDI KWA KASI AACHIA NGOMA MBILI KWA PAMOJA

Mkali katika gemu hapa Tanzania aliyewahi kutingisha na bado anaendelea kutingisha katika gemu la Bongo Flava mkali kutoka Mwanza PNC sasa amerudi tena kwa kasi na ngoma mbili kali akidhihirisha kwamba yeye ni msanii ambae hawezi kupotea na kipaji ni chake alichopewa…
festo and folly bliz

Wednesday 10 July 2013

Clinton amtumia Mandela heri ya kuzaliwa

Rais Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton
BIG 4 MILL BY FESTO ERNESTY,
Johannesburg. Siku chache kabla ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Rais Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton, amemtumia salamu maalumu za kumtakia sherehe njema.
Clinton ambaye ni rafiki wa karibu na familia ya Mandela,  aliyeungana na Dalai Lama na Askofu wa nchi hiyo, Desmond Tutu, walituma  salamu kwa njia ya video kwa vyombo vya habari jana. Julai 18, Mandela anatarajiwa kutimiza miaka 95.
 Mandela, ambaye alilazwa hospitali ya magonjwa ya moyo tangu Juni 8 mwaka huu, anasumbuliwa na ugonjwa wa mapafu. Hata hivyo,  hali inatajwa kuwa siyo mbaya wala nzuri.
Maelfu ya Waafrika Kusini wamekuwa wakiomba usiku na mchana kuomba walau afikie miaka 95. 
Hali hiyo inajionyesha hasa kutokana na watu wengi kufika hospitalini kumtakia kheri, licha ya hali yake kuwa  mbaya.
“Ni taharuki tu hapa, sioni kama kuna hali ya kawaida,” alisema Irene Lambert, Mwalimu mwanafunzi kutoka Johannesburg.
Mwalimu huyo na mpenzi wake, walifika hospitalini hapo wakiwa na picha ya Mandela na kadi yenye ujumbe kwake na kusema: “Tumekuja na ujumbe huu kwa ajili ya Mandela, lakini tutawapa familia kwa kuwa yeye hawezi kuusoma.”

Kenya yaongoza kwa ufisadi


Yaongoza kwa ufisadi kati ya nchi 107 ambako utafiti huo ulifanyika,jambo ambalo limewasikitisha waken

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Transparency International, Kenya imeshika nafasi ya nne kwa ufisadi ikiwa ni  miongoni mwa nchi 107 ambako utafiti huo ulifanyw.
Ripoti hiyo ilibaini kwamba Wakenya saba kati ya 10 waliohojiwa walisema wamewahi kutoa hongo maishani mwao ili waweze kupata huduma moja hadi nane kati ya zilizochunguzwa.
Kulingana na utafiti huo, maofisa wa polisi ndio waliopatikana kuwa mafisadi zaidi nchini wakifuatiwa na wabunge, vyama vya kisiasa, mahakama na wafanyakazi wa Serikali.
Wakenya wengi walisema vyombo vya habari, mashirika yasiyo ya kiserikali na taasisi za kidini hazina ufisadi mwingi.
Nchi fisadi zaidi duniani ni Sierra Leone ambako asilimia 84 ya watu waliohojiwa walikubali kwamba wametoa hongo. Sierra Leone inafuatwa na Liberia (asilimia 75) na Yemen (asilimia 74).
Nchi ambazo zilipatikana kuwa na ufisadi finyu ni Finland, Japan, Australia, Denmark, Uhispania, Canada, Ureno, Uruguay, Norway, New Zealand, Korea Kusini na Malaysia ambako watu zaidi ya 95 kati ya 100 waliohojiwa walisema hawajaona ufisadi wowote nchini mwao.
Katika eneo la Afrika Mashariki, Kenya ndiyo nchi fisadi zaidi ikifuatwa na Uganda (asilimia 61) na Tanzania (asilimia 56). Kulingana na utafiti huo ambao watu 114,000 walihojiwa, Rwanda ilipatikana kuwa na ufisadi mdogo zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Raia 13 pekee kati ya 100 wa nchi hiyo walikubali mwamba wametoa hongo. Ufisadi ulipatikana kukithiri zaidi barani Afrika. Baadhi ya nchi fisadi zaidi Afrika ni Zimbabwe, Msumbiji, Libya na Cameroon (zote zikiwa na asilimia 62) na Nigeria (asilimia 44).

My Blog List