BIG 4 MILL

big4mill.blogspot.com.

Usisite kutembelea blog yako

Karibu nawe mahali popote... - big4mill.blogspot.com.

Tunaishi pamoja wakati wowote

http://www.big4mill.blogspot.com for more info - big4mill.blogspot.com.

Kazi zetu ni...

Tunaelimisha, kuburudisha na kadhalka.

Pata habari mbalimbali

Ndani na nje ya Tanzania/ kitaifa na Kimataifa - big4mill.blogspot.com.

Wednesday 10 July 2013

Clinton amtumia Mandela heri ya kuzaliwa

Rais Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton
BIG 4 MILL BY FESTO ERNESTY,
Johannesburg. Siku chache kabla ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Rais Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton, amemtumia salamu maalumu za kumtakia sherehe njema.
Clinton ambaye ni rafiki wa karibu na familia ya Mandela,  aliyeungana na Dalai Lama na Askofu wa nchi hiyo, Desmond Tutu, walituma  salamu kwa njia ya video kwa vyombo vya habari jana. Julai 18, Mandela anatarajiwa kutimiza miaka 95.
 Mandela, ambaye alilazwa hospitali ya magonjwa ya moyo tangu Juni 8 mwaka huu, anasumbuliwa na ugonjwa wa mapafu. Hata hivyo,  hali inatajwa kuwa siyo mbaya wala nzuri.
Maelfu ya Waafrika Kusini wamekuwa wakiomba usiku na mchana kuomba walau afikie miaka 95. 
Hali hiyo inajionyesha hasa kutokana na watu wengi kufika hospitalini kumtakia kheri, licha ya hali yake kuwa  mbaya.
“Ni taharuki tu hapa, sioni kama kuna hali ya kawaida,” alisema Irene Lambert, Mwalimu mwanafunzi kutoka Johannesburg.
Mwalimu huyo na mpenzi wake, walifika hospitalini hapo wakiwa na picha ya Mandela na kadi yenye ujumbe kwake na kusema: “Tumekuja na ujumbe huu kwa ajili ya Mandela, lakini tutawapa familia kwa kuwa yeye hawezi kuusoma.”

Kenya yaongoza kwa ufisadi


Yaongoza kwa ufisadi kati ya nchi 107 ambako utafiti huo ulifanyika,jambo ambalo limewasikitisha waken

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Transparency International, Kenya imeshika nafasi ya nne kwa ufisadi ikiwa ni  miongoni mwa nchi 107 ambako utafiti huo ulifanyw.
Ripoti hiyo ilibaini kwamba Wakenya saba kati ya 10 waliohojiwa walisema wamewahi kutoa hongo maishani mwao ili waweze kupata huduma moja hadi nane kati ya zilizochunguzwa.
Kulingana na utafiti huo, maofisa wa polisi ndio waliopatikana kuwa mafisadi zaidi nchini wakifuatiwa na wabunge, vyama vya kisiasa, mahakama na wafanyakazi wa Serikali.
Wakenya wengi walisema vyombo vya habari, mashirika yasiyo ya kiserikali na taasisi za kidini hazina ufisadi mwingi.
Nchi fisadi zaidi duniani ni Sierra Leone ambako asilimia 84 ya watu waliohojiwa walikubali kwamba wametoa hongo. Sierra Leone inafuatwa na Liberia (asilimia 75) na Yemen (asilimia 74).
Nchi ambazo zilipatikana kuwa na ufisadi finyu ni Finland, Japan, Australia, Denmark, Uhispania, Canada, Ureno, Uruguay, Norway, New Zealand, Korea Kusini na Malaysia ambako watu zaidi ya 95 kati ya 100 waliohojiwa walisema hawajaona ufisadi wowote nchini mwao.
Katika eneo la Afrika Mashariki, Kenya ndiyo nchi fisadi zaidi ikifuatwa na Uganda (asilimia 61) na Tanzania (asilimia 56). Kulingana na utafiti huo ambao watu 114,000 walihojiwa, Rwanda ilipatikana kuwa na ufisadi mdogo zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Raia 13 pekee kati ya 100 wa nchi hiyo walikubali mwamba wametoa hongo. Ufisadi ulipatikana kukithiri zaidi barani Afrika. Baadhi ya nchi fisadi zaidi Afrika ni Zimbabwe, Msumbiji, Libya na Cameroon (zote zikiwa na asilimia 62) na Nigeria (asilimia 44).

Mghana alivyouawa kinyama Bagamoyo

 
Mbali na Marwa, ambaye amesoma kozi ya urubani, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Peter Charles Mayalla, ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo

Dar es Salaam. Salimu Mohamed Marwa (25) ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara wa magari, raia wa Ghana, Jose ph Opong.
Mbali na Marwa, ambaye amesoma kozi ya urubani, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Peter Charles Mayalla, ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo.
Washtakiwa hawa hao, ambao wote ni wakazi wa Bagamoyo mkoani Pwani wanakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, inayosikilizwa na Jaji Njengafibili Mwaikugile.
Wanadaiwa kuwa Septemba 10, 2010, walimuua kwa makusudi Opong, kwa kumkatakata sehemu mbalimbali za mwili, baada ya kumlewesha kwa dawa za kulevya na kisha kwenda kumzika katika msitu wa Kaole.
Awali Marwa, alitiwa mbaroni kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, baada kukamatwa akiwa na nyaraka za magari ya marehemu Opong katika harakati za kuyauza magari hayo yaliyokuwa Bandarini.
Alikamatwa baada ya mke wa marehemu Opong kutoa taarifa Kituo Kikuu cha Polisi, Septemba 22, kuwa mumewe alikuwa hajaonekana tangu Septemba 9, na kwamba aliondoka kwenda kushughulikia magari yake yaliyokuwa bandarini.
Baada ya taarifa hizo, Polisi walitoa taarifa bandarini kuwa mtu yeyote atakayefika kutaka kutoa magari hayo asiruhusiwe, na Septemba 28, ndipo Salim alipokamatwa akiwa na nyaraka za magari hayo, mkataba wa mauziano na kitambulisho cha marehemu Opong.
Kwanza alipoulizwa kuhusu mahali alipozipata nyaraka hizo alisema kuwa ameuziwa na Joseph Opong, lakini alipoulizwa mahali alikokuwa Opong alijibu kuwa hajui na kwamba baada ya kuuziana, waliachana.
Kuhusu kitambulisho ambacho kilikuwa na jina la Opong lakini kikiwa na picha yake, alishindwa kueleza lolote.
Hivyo kesho yake Septemba 29, timu ya Upelelezi kutoka Polisi Kanda ya Dar es Salaam ikiongozwa na Inspekta (Mkaguzi wa Polisi), Saidi Mohamed Mwagara ilikwenda na mtuhumiwa nyumbani kwake Bagamoyo, kufanya ukaguzi ambao ungewezesha kubaini alikokuwa Opong.
Inspekta Mwagara alidai kuwa hata hivyo katika ukaguzi wao hawakuweza kupata kielelezo chochote cha kuwasaidia, na kwamba wakati wakiwa kwa mtuhumiwa huyo, alimtaka mtuhumiwa awaeleze ukweli kwa kuwa walikuwa wameshachoka
.
Alidai kuwa mshtakiwa huyo alisema naye ameshachoka kuzunguka na kwamba sasa anataka awaeleze ukweli, na ndipo akasema kuwa Opong tayari wameshamuua, na kwamba yuko tayari kwenda kuwaonyesha walikomzika.

Monday 8 July 2013

QUEEN DARLEEN: KWENYE MAPENZI UBABE NAUWEKA PEMBENI

Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’.

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’ amesema pamoja na…

NEW AUDIO: WYNEM - "MWANAMBUZI"

Msanii anayekuja kwa kasi katika muziki wa Bongo Flava hapa nchini Tanzania, ambae pia amaeshafanya colabo na wasanii wakali katika gemu akiwemo Linex, Suma Mnazareth, Nick Maujanja na wengineo muite Wynem jina halisi anaitwa Mahamud Issa. Gemu la muziki wa kizazi…

Thursday 4 July 2013

FBI wakagua ofisi ya Kova kwa mbwa


 

. Ofisa mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), akiwa na mbwa jana aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya ukaguzi.
Tukio hilo lilitokea muda mfupi kabla ya msafara wa magari ya Marekani kupita yakitokea Ikulu kwenda Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kumlaki Rais Barack Obama.
Polisi ambaye hakutaka kutajwa alisema ofisa huyo  aliingia na mbwa hadi maeneo ya mapokezi, lakini muda mfupi walitoka.
“Walikwenda moja kwa moja mapokezi wakafanya ukaguzi,  kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza:
“Licha ya mimi kutokuwa na  cheo pale, lakini hili la kutukagua na mbwa, ni kama wametudhalilisha... sisi ndiyo tunaaminika kwa usalama, leo hii wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu.”
Hata hivyo, usalama kwenye vituo vingi ikiwamo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusu Nyerere, vilikuwa chini ya usimamizi na uangalizi wa makachero wa Marekani.

Mandla: Mjukuu anayeinyima usingizi familia ya Mandela


Mjukuu wa Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Mandla Zwelivelile Mandel

Johannesburg. Mjukuu wa Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Mandla Zwelivelile Mandela ambaye ameibua mgogoro mkubwa katika familia ya shujaa huyo wa Afrika katika mzozo wa makaburi amekuwa na mlolongo wa visa katika maisha yake.
Visa hivyo kwa sehemu kubwa vinahusu maisha yake ya ndoa kwani ameoa na kuacha mara tatu huku akikabiliwa na kisa kingine cha kudaiwa kuuza haki za televisheni za kuonyesha mazishi ya Mzee Mandela.
Mandla ambaye jana aliamriwa na Mahakama kurejesha mabaki ya miili ya watoto watatu wa Mandela, alizaliwa mwaka 1974 na kwa sasa ni Chifu wa eneo la Mvezo. Ni msomi mwenye shahada ya kwanza ya siasa aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Rhodes mwaka 2007.
Chifu huyo wa Kabila la Xhosa amekuwa na vituko vingi katika maisha yake. Mwaka 2009 alizua utata baada ya kuuza haki ya kutangaza mazishi ya Mandela atakapokufa kwenye kituo cha televisheni cha SABC kwa Rand 3 milioni (Sh481 milioni).
Hata hivyo, suala hilo lilifikishwa katika Mahakama Kuu ya Mthatha ambako hukumu ilitoka na alipewa siku 15 kutangaza kama kweli ameuza haki ya matangazo ya mazishi ya Mandela au akanushe taarifa hizo.
Taarifa zilisema kuwa kutokana na shinikizo la baadhi ya wanafamilia na mkazo wa hukumu ya Mahakama, Mandla alilazimika kukanusha kuuza haki ya matangazo ya mazishi ya Mandela kwa kituo kimoja cha televisheni.
Mandla ambaye ni mtoto wa Makgatho Mandela aliyefariki dunia mwaka 2005 baada ya kuugua maradhi yanayofanana na ya Ukimwi, alipata hadhi ya uchifu baada ya kifo cha baba yake mwaka 2007.
Mandela ambaye alikabidhiwa uchifu wa uongozi wa watu wa Kabila la Xhosa takriban miaka 70, ndiye aliyempendekeza Mandla kuchukua wadhifa huo. Alikabidhiwa wadhifa huo mwaka 2007 wakati huo akiwa na umri wa miaka 32. Majukumu yake yalikuwa kuongoza sherehe za kimila, kutatua matatizo ya ndani ya ukoo wao na kuwakilisha Kabila la Xhosa katika masuala ya kisiasa.
Kutokana na majukumu hayo, Mandla alichaguliwa kuwa mbunge mwaka 2009 kupitia Chama cha African National Congress (ANC). Mke wake wa kwanza ni Tando Mabuna-Mandela aliyemuoa mwaka 2004. Hata hivyo, mwaka 2009, mwanamke huyo aliomba talaka mahakamani akidai kuwa mumewe huyo ni mgumba.
Mke wa pili wa Mandla ni Anais Grimaud aliyezaliwa mwaka 1990 huko Reunion ambaye alibadili jina lake na kuitwa Nkosikazi Nobubele. Walioana Machi 2010 katika ndoa ya kimila.
Septemba 2011 alipata mtoto aliyepewa jina la Qheya II Zanethemba Mandela na alikaribishwa kwa Mandela kijijini Qunu kwa taratibu za kimila. Hata hivyo, Agosti mwaka 2012, Mandla alimkataa mtoto huyo akidai mkewe alikuwa ana uhusiano na kaka yake, kesi ilifika mahakamani na waliachana kutokana na sababu hiyo.
Mkewe wa tatu ni Nodiyala Mbali Makhathini ambaye walioana Desemba 24, 2011, lakini tayari amefungua kesi ya kudai talaka.

Michelle Obama: Acheni kufuatilia mavazi yangu

“Watu wanapaswa kuelewa, wake za marais nao hufanya mambo mazuri ya jamii na kazi yao siyo kubadili staili za nywele na mavazi tu,” Michelle Obama
Dar es Salaam. Michelle Obama na Laura Bush walikuwa kivutio jana kwenye Mkutano wa wake wa marais wa Afrika unaoendelea Dar es Salaam, pale walipoongelea kwa mzaha jinsi vyombo vya habari vinavyoshupalia kuandika kuhusu staili za nywele na  mavazi ya wake wa marais, huku vikiacha masuala ya msingi.
Mkutano huo uliofunguliwa jana na Rais Jakaya Kikwete, ni maalumu kwa ajili ya kusaidia wanawake wajasiriamali wa Afrika, unatarajiwa kumalizika leo
.
Wakizungumza kwenye mjadala ulioongozwa na Mwandishi wa Habari wa Marerkani, Cokie Roberts,  Michelle, ambaye ni mke wa Rais wa Marekani, Barack Obama, alisema alifurahia kupata nafasi ya kufanya majadiliano na Laura, ambaye ni mke wa Rais wa zamani wa Marekani.
“Ninampenda mwanamke huyu,” alisema Michelle kwa utani kama vile hamfahamu.  
“Sishangai sana maana tuko klabu moja nadhani,”  alijibu Laura kwa utani akiwa na maana kuwa,  wao wote wana uzoefu wa kuwa wake wa marais.
“Unajua tunaishi maisha ya shida, maana wenzetu wa habari wanaangalia zaidi staili za mavazi na nywele zetu badala ya kuangalia mambo ya msingi,” alisema Michelle.

 

 Alisema mwanzoni mwa mwaka huu, alibadili staili ya nywele lakini alishangaa jinsi suala hilo lilivyokuzwa na vyombo vya habari.

Pinda aisaliti kauli yake, aruhusu tena sherehe


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, 
Dodoma. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amewaagiza Watanzania kuwa na uzalendo wa kuwaenzi na kuwakumbuka wenzao ambao wamefanya kazi  muda mrefu kwa kuthamini mchango wao.
Pinda alitoa kauli hiyo juzi katika viwanja vya Bunge, aliposhiriki hafla ya kuwaaga wafanyakazi waliostaafu utumishi na wale waliohamishwa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuanzia 2010.
Hata hivyo, Pinda alisema  yeye ndiye aliyemwagiza Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia kuandaa hafla hiyo ili kuwatunuku zawadi na kula nao chakula pamoja na watumishi hao, ambao idadi yao ilikuwa 59 kutoka sehemu mbalimbali nchini. Hata hivyo walihudhuria 35.
Juzi ilikuwa ni siku ya pili mfululizo kwa Pinda kushirikia warsha katika viwanja hivyo, siku iliyotangulia alikuwa ameshiriki  sherehe kubwa iliyoandaliwa na Bunge kumwaga Spika Mstaafu ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye alitumikia nafasi ya Uspika kwa miaka mitano 2005/10.
 Sherehe ya juzi ambayo iliandaliwa kwa agizo la Pinda, inapingana na kauli na maagizo yake ambayo amekuwa akitoa kwa nyakati tofauti kwamba, makongamano na warsha zisizo na tija ni ufujaji fedha za umma.
“Mimi ndiye niliyeamua kufanya hivi na huu ni ubinadamu tu nikaona nimtume mama Ghasia afanye maandalizi hayo, lengo kuu la hapa ni kukaa pamoja na wenzetu na kuwaambia kuwa tunashukuru kwa kazi yenu nzuri na pia tunathamini michango yenu,” alisema Pinda.
Alisema huo ulikuwa ni mwanzo, lakini Tamisemi itakuwa ikifanya hivyo kila mwaka  kuwaaga watu wanaostaafu na wanaohamia wizara zingine.
Kuhusu wastaafu hao, alisema Serikali inapaswa kuwathamini na kutambua michango yao wakati wote kuliko kuwatelekeza kama ilivyo sasa.
Alisema kustaafu kwa mtu sio kwamba anakuwa amepungukiwa hekima na maarifa, bali ni utaratibu ukifika wakati fulani anatakiwa kupumzika.
Licha ya hilo,  aliwaagiza viongozi wa Tamisemi kuangalia uwezekano wa kuwasaidia watu wanaojiandaa kustaafu ili wajenge nyumba za kufikia na familia zao, kwani wengine humaliza muda  na kushindwa  kujenga. 
Tangu kuingia ateuliwe, Pinda amekuwa akipiga vita sherehe na ununuzi wa magari ya kifahari kwa madai kuwa, ni ubadhirifu wa fedha za umma.
Hatua hiyo inaonyesha ameanza kubariki fedha hizo kufanya sherehe.

Tuesday 2 July 2013

DIMOND KTK SPORAN SHOW

diamond platinum with sporah

 da prezident aka sukari ya warembo mwenyewe anajiita  sugar
 with da crew
 WASAAAAAFI
Photo: THE PRESIDENT MWENYEWE DIAMOND NDANI YA SPORAH SHOW STUDIO
HAWA NDIO MANIGAZ WA DIAMOND

BLOG YA NESTY BOY TWIST YAMNASA WEMA JINSI ALIVO JIPIGA TATOO

ni mtoto wema akiwa ktk harakati za kuamka.lakinBIG 4 MILLyamnasa jinsi alivo jipiga tatoooo

KATIKA BLOG YA NESTY BOY TWIST.DIAMOND AONESHA HADHARANI SIMU ZAKE ZA GARAMA

huyu  ndiye diamond mijisimu anayo tumia ni garama tupu .ni mamkwanja tuuuuuuuuuu yaliyo mjaaaa.BIG 4 MILL.0718718290.

Maelfu wajitokeza barabarani kumuaga Rais Obama


Rais Obama akiwaaga watanzania waliofika katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  

Dar es Salaam. Rais wa Marekani Barack Obama amehitimisha ziara yake ya Afrika mapema leo, kwa kutembelea mradi wa uzalishaji umeme wa Symbion Ubungo, jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake Ubungo, Rais Obama alielezea jinsi mkakati wa serikali yake wa kuhakikisha Afrika inapata umeme utakavyoboresha maisha ya wakazi wa bara hili.
Mapema leo asubuhi, Rais Obama aliungana na Rais wa zamani wa Marekani George Bush kuweka shada la maua kuwakumbuka wahanga wa shambulizi la kigaidi la ubalozi wa Marekani mwaka 1998.
Katika ziara yake ya siku mbili iliyoanza jana nchini Tanzania, Rais Obama amesisitiza umuhimu wa kuboshesha mahusiano ya kibiashara kati ya Afrika na Marekani.
Wakati wa ziara yake, Obama aliahidi kutilia mkazo vipaumbele vinne vya Marekani kwa Tanzania.
Marekani itaisaidia serikali ya Kikwete kuboresha miradi mbalimbali ya umeme, miundombinu ya barabara, maji na programu za kielimu kwa  vijana kwa lengo la kuongeza ajira.
Jijini Dar es salama, Barabara za Ally Hassan Mwinyi, Mandela, Sam Nujoma na ile ya Morogoro zilifungwa kwa muda kuanzia majira ya saa tatu asubuhi huku maelfu ya wananchi wakitanda barabarani kwa lengo la kumuaga rais huyo
.
Mara baada ya kufika katika  uwanja wa Ndege Rais Obama na Mkewe walitumia  muda mfupi kuagana na mwenyeji wao Rais Kikwete na mkewe ikiwa ni pamoja na kuwaaga mamia ya viongozi waliofika uwanjani hapo.

Mikakati ya Marekani Afrika

Kiongozi huyo aliwasili Dar es Salaam jana mchana ikiwa ni nchi ya mwisho katika ziara yake barani Afrika ikitanguliwa na Senegal na Afrika Kusini
.
Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais Jakaya Kikwete Ikulu, Rais Obama alisema aliainisha mambo hayo wakati alipozungumza na mwenyeji wake huyo.
Alisema katika mazungumzo hayo, waligusia mradi wa mkubwa wa umeme uitwao Power Afrika wenye lengo la kuongeza kiwango cha umeme kinachozalishwa nchini na barani Afrika ili kupata umeme nafuu na wa uhakika utakaochagiza kuongeza uzalishaji na kukuza ajira.

My Blog List