Wednesday 10 July 2013

Mghana alivyouawa kinyama Bagamoyo

 
Mbali na Marwa, ambaye amesoma kozi ya urubani, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Peter Charles Mayalla, ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo

Dar es Salaam. Salimu Mohamed Marwa (25) ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara wa magari, raia wa Ghana, Jose ph Opong.
Mbali na Marwa, ambaye amesoma kozi ya urubani, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Peter Charles Mayalla, ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo.
Washtakiwa hawa hao, ambao wote ni wakazi wa Bagamoyo mkoani Pwani wanakabiliwa na kesi hiyo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, inayosikilizwa na Jaji Njengafibili Mwaikugile.
Wanadaiwa kuwa Septemba 10, 2010, walimuua kwa makusudi Opong, kwa kumkatakata sehemu mbalimbali za mwili, baada ya kumlewesha kwa dawa za kulevya na kisha kwenda kumzika katika msitu wa Kaole.
Awali Marwa, alitiwa mbaroni kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, baada kukamatwa akiwa na nyaraka za magari ya marehemu Opong katika harakati za kuyauza magari hayo yaliyokuwa Bandarini.
Alikamatwa baada ya mke wa marehemu Opong kutoa taarifa Kituo Kikuu cha Polisi, Septemba 22, kuwa mumewe alikuwa hajaonekana tangu Septemba 9, na kwamba aliondoka kwenda kushughulikia magari yake yaliyokuwa bandarini.
Baada ya taarifa hizo, Polisi walitoa taarifa bandarini kuwa mtu yeyote atakayefika kutaka kutoa magari hayo asiruhusiwe, na Septemba 28, ndipo Salim alipokamatwa akiwa na nyaraka za magari hayo, mkataba wa mauziano na kitambulisho cha marehemu Opong.
Kwanza alipoulizwa kuhusu mahali alipozipata nyaraka hizo alisema kuwa ameuziwa na Joseph Opong, lakini alipoulizwa mahali alikokuwa Opong alijibu kuwa hajui na kwamba baada ya kuuziana, waliachana.
Kuhusu kitambulisho ambacho kilikuwa na jina la Opong lakini kikiwa na picha yake, alishindwa kueleza lolote.
Hivyo kesho yake Septemba 29, timu ya Upelelezi kutoka Polisi Kanda ya Dar es Salaam ikiongozwa na Inspekta (Mkaguzi wa Polisi), Saidi Mohamed Mwagara ilikwenda na mtuhumiwa nyumbani kwake Bagamoyo, kufanya ukaguzi ambao ungewezesha kubaini alikokuwa Opong.
Inspekta Mwagara alidai kuwa hata hivyo katika ukaguzi wao hawakuweza kupata kielelezo chochote cha kuwasaidia, na kwamba wakati wakiwa kwa mtuhumiwa huyo, alimtaka mtuhumiwa awaeleze ukweli kwa kuwa walikuwa wameshachoka
.
Alidai kuwa mshtakiwa huyo alisema naye ameshachoka kuzunguka na kwamba sasa anataka awaeleze ukweli, na ndipo akasema kuwa Opong tayari wameshamuua, na kwamba yuko tayari kwenda kuwaonyesha walikomzika.

0 comments:

Post a Comment

My Blog List