BIG 4 MILL

big4mill.blogspot.com.

Usisite kutembelea blog yako

Karibu nawe mahali popote... - big4mill.blogspot.com.

Tunaishi pamoja wakati wowote

http://www.big4mill.blogspot.com for more info - big4mill.blogspot.com.

Kazi zetu ni...

Tunaelimisha, kuburudisha na kadhalka.

Pata habari mbalimbali

Ndani na nje ya Tanzania/ kitaifa na Kimataifa - big4mill.blogspot.com.

Tuesday 11 June 2013

Kagasheki, Lembeli wapingana kwa takwimu

Share bookmark Print Email Rating
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki 
Na Hakimu Mwafongo  (email the author)

Posted  Jumanne,Juni11  2013  saa 21:39 PM
Kwa ufupi
  • Taarifa za Serikali kuwa tembo 10,000 wanauawa kila mwaka si sahihi kwa kuwa zimeandaliwa na maofisa wa Serikali kwa ajili ya kuwatetea.
SHARE THIS STORY
0
Share


Iringa. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, James Lembeli amepinga kauli zilizotolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki kuhusu tembo wanaouawa nchini kutokana na ujangili.
Waziri Kagasheki alisema kuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Tawiri, zaidi ya tembo 10,000 huuawa kila mwaka na majangili kitu ambacho kinatishia maisha ya wanyama hao hapa nchini.
Kagasheki alisema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa Waandishi wa habari wa Vyombo vya Habari nchini na Shirika la Hifadhi za Taifa(Tanapa) uliofanyika Iringa jana.
Hata hivyo Lembeli alisema kiasi kilichosemwa na Waziri ni kidogo kwa kuwa watafiti waliotoa takwimu hizi ni wa Serikali hivyo wanaficha baadhi ya mambo.
“Taarifa za Serikali kuwa tembo 10,000 wanauawa kila mwaka si sahihi kwa kuwa zimeandaliwa na maofisa wa Serikali kwa ajili ya kuwatetea,” alisema Lembeli.
Alisema tatizo la ujangili wa meno ya tembo nchini ni kubwa na idadi inayotolewa ni kwa wale tembo wanaouawa kwenye hifadhi tu wakati wengi bado wanauawa na majangili nje ya hifadhi za Taifa.
Aidha aliwataka wanahabari kutokuwa waoga katika kufichua habari za majangili wa meno ya tembo kwa kuwa wanaojihusisha na meno ni watu wenye uwezo mkubwa kifedha na wana mitandao mikubwa.
“Ni vyema wanahabari kutokuwa waoga katika kufichua mitandao ya ujangili kwa kuwa wanaohusika wana fedha na kuna viongozi ambao wanawaunga mkono”, alisema Lembeli.
Akizungumzia umuhimu wa vyombo vya habari Kagasheki alivitaka kuisaidia Serikali kukabiliana na vita dhidi ya ujangili wa tembo na wanyamapori wengine.
Aliwaomba waandishi wa habari kusaidia kwa kuwa kuna rushwa bandarini, viwanja vya ndege, ndani ya Mahakama, serikalini, polisi, idara ya usalama, na mamlaka ya mapato ndiyo maana ujangili hasa wa meno ya tembo unaongezeka.
Alisema watalii havutii kuwaona tembo wanaoendelea kupungua duniani kote kutoka milioni 50 mwaka 1930 hadi 402,067 mwaka jana.
Kagasheki alisema kwa upande wa Tanzania idadi yake imepungua kutoka kati ya tembo 250,000 na 300,000 katika miaka ya sitini hadi hadi 110,000 mwaka 2009


Marekani yataja sababu nne za Obama kuja Tz


 

  • Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
SHARE THIS STORY



Dar es Salaam. Marekani imetaja sababu nne ambazo zimemfanya Rais Barrack Obama kuijumuisha Tanzania katika ziara yake ya bara la Afrika.
Rais Obama amepanga kulitembelea bara la Afrika kuanzia Juni 26 hadi Julai 3, mwaka huu na atazitembelea pia Senegal na Afrika Kusini.
Kiongozi huyo wa Marekani ambaye baba yake mzazi ni mzaliwa wa Kenya, anatarajiwa kuwasili nchini Julai Mosi kwa ziara ya siku tatu. Atakuwa Rais wa tatu wa Marekani kuitembelea Tanzania baada ya Bill Clinton mwaka 2000 na George Bush mwaka 2008.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Balozi wa Marekani, Alfonso Lenhardt alisema sababu ya kwanza ya Obama kuja Tanzania ni kutokana na kuwa mfano wa utawala bora, demokrasia na ushirikishaji wa watu wake wakati wa kufanya uamuzi unaogusa maisha yao ya kila siku.
Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya mfano linapokuja suala la uongozi bora na ndiyo maana imekuwa na amani na utulivu kwa muda mrefu ikilinganishwa na nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
“Nchi nyingi za Afrika zinazoizunguka Tanzania zimekuwa na matatizo ya vita vya wenyewe na hata ukosefu wa utawala bora,” alisema Balozi Lenhardt ingawa alidokeza kuwa katika siku za karibuni imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na matukio ya uvunjifu wa amani.
Balozi Lenhardt alisema sababu nyingine inayomfanya Rais Obama kuja Tanzania ni kutokana na jitihada za Serikali ya Marekani kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kasi ya ukuaji wa uchumi.
“Rais Obama anakuja kuunga mkono juhudi za Watanzania katika kutengeneza mazuri ya uwekezaji lakini bila kusahau kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeivutia Serikali ya Marekani,” alisema.
Balozi Lenhardt alitaja sababu nyingine inayomleta Rais Obama kuwa ni kuisaidia Tanzania kuendeleza fursa mbalimbali za kujiletea maendeleo.
Alisema uendelezaji huo wa fursa una lengo la kuisaidia Serikali ya Tanzania kukabiliana na tatizo la umaskini.
Alisema Marekani ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa fedha nyingi za misaada na akisema kwa mfano, mwaka 2012 pekee ilitoa Dola 750 milioni.
Aidha, alisema nchi yake imekuwa ikitoa misaada mingi kupitia Shirika la Millenium Challenge (MCC), ambayo imejikita zaidi katika kusaidia sekta za umeme, maji na miundombinu.

Baada ya Maojiano na Bongo5 Diamond alisema kwamba alishindwa kuhudhuria mashindano hayo kwa sababu alikua katika uzinduzi wa kinyaj kipya cha Novida kutoka katika Kampuni ya vinyaji Coca cola hapa Tanzania na imeweza kufanya balozi wa kinyaji hicho. Hiyo ndiyo sababu iliyomfanya star wa Bongo Flava Diamond kutokuhudhuria Tuzo hizo ambapo yeye pia alikuwa mshindi wa tuzo wakadha wakadha.

Re-Ranking the NBA's Top 50 Players, 2013 Finals Edition...

Hi-res-169569367_crop_650x440 Mike Conley and Tony Parker both showed off their skills during the postseason.
Ronald Martinez/Getty Images
.
These rankings are based primarily on the events of the 2012-13 campaign. Past events and trends have been taken into account, but they're still secondary concerns. We can't work exclusively based on this season, or else we'd be ranking seasons rather than players.

Sunday, June 9, 2013

KALA JEREMIAH, OMMY DIMPOZ HATIMAYE WAINUKA KIDEDEA PIA WAFUNIKA KILI MUSIC AWARDS 2013

DAR ES SALAAM, Tanzania HATIMAYE kitendawili cha nani kavuna nini katika kinyang’anyiro Kilimanjaro Tanzania Music Awards KTMA 2013, kilipata jibu usiku wa jana, ambapo kategori 37 za mchakato huo zilipata washindi, huku wasanii Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz wakifunika kwa upande wa muziki wa kizazi kipya. Kala Jeremiah aliyekuwa karibu atwae tuzo, alijikuta akimaliza kwa kutwaa tuzo tatu za Wimbo Bora wa Mwaka (Dera God), Msanii Bora wa Hip Hop na ile ya Mtunzi Bora Bora wa Hip Hop, huku akiipoteza ya Wimbo Bora wa Mwaka wa Hip Hop (Dear God) iliyochukuliwa na Nay wa Mitego kuptia wimbo Nasema Nao. Kwa upande wa Dimpoz, nyota pekee aliyekuwa akiwania tuzo saba katika kinyang’anyiro hicho, alipata tuzo tatu za Wimbo Bora wa Bongo Pop (Me and You feat Vanessa Mdee), kibao kilichompa pia tuzo ya Wimbo Bora wa Ushirikiano. Dimpoz akapokea tuzo ya tatu ya Video Bora ya Mwaka kupitia kibao cha Baadae, huku akiangukia pua katika kategori nne za Wimbo Bora wa Mwaka, Msanii Bora wa Mwaka wa Kiume, Msanii Bora wa Mwaka wa Kiume – Bongo Flava na Mtunzi Bora wa Mashairi – Bongo Flava. Katika namna iliyowavutia wengi, Dimpoz aliitoa kwa Vanessa Mdee moja ya tuzo mbili alizoshinda kupitia kibao alichomshirikisha cha Me and You kwa, tukio lililotafsiriwa kama ‘kumpoza’ binti huyo aliyeangukia pua katika kategori ya Msanii Bora Anayechipukia, ambayo ilienda kwa Ali Nipishe. Bendi ya Mashujaa waliibuka kidedea zaidi katika mchakato huo, baada ya kujizolea tuzo tano, kupitia mbili za bendi (Wimbo Bora wa Bendi – Risasi Kidole) na Bendi Bora ya Mwaka, huku ikitwaa tatu za wasanii wake, ambao ni Chalz Baba aliyetwaa mbili za Mtunzi Bora wa Mashairi – Bendi na Msanii Bora wa Kiume – Bendi. Pia rapa wake Ferguson aliibuka kidedea katika kategori ya Rappa Bora wa Bendi, alikowabwaga Greyson Semsekwa, J4, Jonico Flower na Sauti ya Radi. Ukiondoa washindi wa Kategori 35, KTMA 2013 ilitoa tuzo mbili maalum; moja ya All of Fame ilitwaliwa na kundi la Kilimanjaro Band ‘Wana Njenje’ ambayo ilipokelewa na Waziri Ali, huku ile ya Individual All of Fame ikinyakuliwa na nyota wa muziki wa zamani marehemu Salum Abdallah na kupokelewa na mwanaye. Hapa tunakuletea kategori zote 35. Wimbo Bora wa Mwaka; Dear God - Kala Jeremiah Msanii Bora wa Kiume; Diamond Platnumz Msanii Bora wa Kike; Lady Jaydee ‘Comandoo’ Msanii Bora wa Kike wa Taarab; Isha Mashauzi Msanii Bora wa Kiume wa Taarab; Mzee Yusuf Msanii Bora wa Kiume Bongo Flava; Diamond Platnumz Msanii Bora wa Kike Bongo Flava; Recho Msanii Bora wa Hip Hop; Kala Jeremiah Msanii Bora wa Kiume Bendi; Chalz Baba Msanii Bora wa Kike Bendi; Luiza Mbutu Msanii Bora Anayechipukia; Ali Nipishe Video Bora ya Mwaka; Baadae - Ommy Dimpoz Mtunzi Bora wa Taarab; Thabit Abdul Mtunzi Bora wa Bongo Flava; Ben Pol Mtunzi Bora wa Mashairi Hi Hop; Kala Jeremiah Mtunzi Bora wa Mashairi Bendi; Chalz Baba Mtayarishaji Bora wa Mwaka Bongo Flava; Man Water Mtayarishaji wa Wimbo wa Mwaka Taarab; Enrico Mtayaraishaji wa Wimbo wa Mwaka Bendi; Amoroso Mtayarisha Bora Anayechipukia; Mensen Selecta Rapa Bora wa Mwaka - Bendi; Fagasoni Wimbo Bora wa Asili ya Kitanzania; Chocheeni kuni - Mrisho Mpoto Feat Ditto Wimbo Bora wa Mwaka - Bendi; Risasi kidole - Mashujaa band Wimbo Bora wa Mwaka - Reggae; Kilimanjaro - Warriors from The East Wimbo Bora wa Afrika Mashariki; Valu Valu - Jose Chameleone Wimbo Bora wa Mwaka Bongo Pop; Me and you - Ommy Dimpoz Feat Vanessa Mdee Wimbo Bora wa Ushirikiano; Me and U - Ommy Dimpoz Feat Vanessa Mdee Wimbo Bora wa Hip Hop; Nasema Nao - Nay wa Mitego Wimbo Bora wa Mwaka wa RnB; Kuwa na Subira - Rama Dee Feat Mapacha Wimbo Bora wa Mwaka wa Ragga/Dancehall; Predator - Dabo Wimbo Bora wa Mwaka wa Taarab; Mjini chuo kikuu - Khadija Kopa Wimbo Bora wa Mwaka Zouk/Rhumba; Ni wewe - Amini Bendi Bora ya Mwaka; Mashujaa Band Kundi Bora la Mwaka la Taarab; Jahazi Modern Taarab Kundi Bora la Mwaka Bongo Flava; Jambo squadBIG 4 MILL

My Blog List