BIG 4 MILL

big4mill.blogspot.com.

Usisite kutembelea blog yako

Karibu nawe mahali popote... - big4mill.blogspot.com.

Tunaishi pamoja wakati wowote

http://www.big4mill.blogspot.com for more info - big4mill.blogspot.com.

Kazi zetu ni...

Tunaelimisha, kuburudisha na kadhalka.

Pata habari mbalimbali

Ndani na nje ya Tanzania/ kitaifa na Kimataifa - big4mill.blogspot.com.

Sunday 9 June 2013


SHARE THIS STORY
0
Share


Dar. Msanii wa muziki wa miondoko ya R’n’B, Benard Paul maarufu kama Ben Pol wiki hii anatarajia kuachia video ya wimbo wake mpya unaoitwa Jikubali ambao ameutoa wiki iliyopita .
Mbali na hilo, Ben Pol ameeleza kuwa siri ya yeye kuingia kwenye vipengele vitano katika tuzo muziki za Kilimanjaro mwaka huu ni kutokana na kazi nzuri anazozifanya ambazo mashabiki wanazikubali na hakuna kingine hivyo alistahili
Aliliambia Mwananchi mwisho wa wiki kuwa mwaka huu umekuwa wenye mafanikio kwake, kwani toka aanze muziki hakutarajia kama ipo siku ataangiza nyimbo kwenye vipengele vingi.
 
 
“Mwaka juzi (2011) niliingiza wimbo mmoja na mwaka jana nyimbo mbili, hapo utaona jinsi gani ninavyopiga hatua kutoka kwenye nyimbo hizo hadi kufikia kuingiza nyimbo tano mwaka huu.
Kwa hakika hili ni jambo la kujivunia , nawashukuru Watanzania kwa msaada wao,” anasema.
Katika hatua nyingine, msanii huyoamewaomba Watanzania wasisite kumpigia kura kwenye kinyang’nyiro hicho ili aweze kunyakuwa tuzo hizo mwaka huu na hatimaye aweke historia ya kuwa msanii wa kwanza wa RnB kunyakua tuzo nyingi.

Nembo za TRA kusaidia sanaa


Wema Sepetu 0

Dar. Kilio cha muda mrefu cha wasanii wa filamu kuibiwa kazi zao kitaisha baada utaratibu wa kuweka nembo za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwenye mikanda ya filamu kuanza Julai, Mosi, mwaka huu.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Maktaba za Video Tanzania, Richard Kalinga alisema hayo Ijumaa iliyopita kwamba kuwekwa kwa nembo hiyo ya TRA itasababisha kazi ya kuwatafuta wanaoiba kazi za wasanii kuwa rahisi.
Alisema hayo kwenye mkutano wa wadau wa filamu ulioandaliwa kwa ajili ya kulinda haki za wasanii wa filamu dhidi ya waharamia na kuifanya sekta hiyo kulipa kodi katika serikali.
Taasisi ya BEST-AC kwa kushirikiana Indigo –MTPC na Media for Development International (MFDI) ndiyo walioitisha mkutano kwa ajili ya kusaidia kuondokana na uharamia wa kazi za wasanii wa filamu.
Kalinga alisema katika utaratibu huo, kazi za filamu zitanunuliwa zikiwa na nembo ya TRA, “mnunuzi akiona mkanda wa filamu anaotaka kuununua hauna nembo hiyo afahamu kwamba huo siyo halisi.
“Mteja akinunua filamu ya aina hiyo afahamu kwamba haitakuwa bora kwa sababu itakuwa imetengenezwa kiholela na kodi ya serikali wanaikwepa,” alisema Kalinga.

Msanii bongo movie aliyeanza kucheza ulaya


 

Kama utakuwa shabiki na mtazamaji mzuri wa filamu za bongo movie, jina la Lucy Francis Komba halitakuwa jipya masikioni mwako.
Msanii huyu alianza sanaa katika Kundi la Kaole, akishiriki baadhi ya vipindi vya televisheni na baadaye kujiunga na Kikundi cha , Dar Talent ambapo alishiriki filamu moja ya vichekesho
.
Katika sanaa, Lucy ameshacheza filamu zaidi ya 50 zikiwemo nne alizocheza nje ya nchi. Filamu ya kwanza aliyocheza nyota huyu na kuonyesha kipaji chake inafahamika kama Utata. Baadaye alishiriki filamu ya Yolanda, Division of Love, Jeraha la Ndoa, Talaka Wodini, Siri ya Moyo Wangu, Teke la Mama, Richmond, Swadakta na nyinginezo
Kwa sasa Lucy ni mwigizaji wa filamu, mwongozaji, mtunzi wa stori na mtayarishaji wa filamu aliyefanikiwa kuvuka mipaka ya nchi hasa Bongo Movie akichanua hadi katika nchi za Burundi, Sierra Leone na Denmark.
Lucy kwa sasa anasubiri kuzindua filamu yake mpya aliyoichezea nchini Denmark.
”Nilienda kupumzika tu, lakini baada ya kuona wana mwitikio mzuri na filamu zetu, ilinibidi nicheze filamu niliyoipa jina la ‘Tanzania to Denmark’,” anasema Lucy.
Anabainisha kuwa filamu hiyo amecheza kwa gharama zake akishirikiana na Kampuni ya Vad Production ya Denmark inayojihusisha na uzalishaji wa filamu.
“Walinisaidia sana hadi hatua ya mwisho. Natarajia kuizindua mwezi huu wa Juni nchini Denmark, naamini itauza sana, maana nimecheza na wasanii maarufu wa huko,”anasema Lucy.
Aprili mwaka jana, msanii huyo alifanikiwa kwenda nchini Ghana kwa maa
ndalizi ya kucheza filamu yake, hata hivyo hakuweza kufanikiwa baada ya msanii mwenzake Kanumba kufariki dunia.
..........................................................................................................................................................

My Blog List