Thursday 4 July 2013

Michelle Obama: Acheni kufuatilia mavazi yangu

“Watu wanapaswa kuelewa, wake za marais nao hufanya mambo mazuri ya jamii na kazi yao siyo kubadili staili za nywele na mavazi tu,” Michelle Obama

Dar es Salaam. Michelle Obama na Laura Bush walikuwa kivutio jana kwenye Mkutano wa wake wa marais wa Afrika unaoendelea Dar es Salaam, pale walipoongelea kwa mzaha jinsi vyombo vya habari vinavyoshupalia kuandika kuhusu staili za nywele na  mavazi ya wake wa marais, huku vikiacha masuala ya msingi.
Mkutano huo uliofunguliwa jana na Rais Jakaya Kikwete, ni maalumu kwa ajili ya kusaidia wanawake wajasiriamali wa Afrika, unatarajiwa kumalizika leo
.
Wakizungumza kwenye mjadala ulioongozwa na Mwandishi wa Habari wa Marerkani, Cokie Roberts,  Michelle, ambaye ni mke wa Rais wa Marekani, Barack Obama, alisema alifurahia kupata nafasi ya kufanya majadiliano na Laura, ambaye ni mke wa Rais wa zamani wa Marekani.
“Ninampenda mwanamke huyu,” alisema Michelle kwa utani kama vile hamfahamu.  
“Sishangai sana maana tuko klabu moja nadhani,”  alijibu Laura kwa utani akiwa na maana kuwa,  wao wote wana uzoefu wa kuwa wake wa marais.
“Unajua tunaishi maisha ya shida, maana wenzetu wa habari wanaangalia zaidi staili za mavazi na nywele zetu badala ya kuangalia mambo ya msingi,” alisema Michelle.

 

 Alisema mwanzoni mwa mwaka huu, alibadili staili ya nywele lakini alishangaa jinsi suala hilo lilivyokuzwa na vyombo vya habari.

0 comments:

Post a Comment

My Blog List