BIG 4 MILL

big4mill.blogspot.com.

Usisite kutembelea blog yako

Karibu nawe mahali popote... - big4mill.blogspot.com.

Tunaishi pamoja wakati wowote

http://www.big4mill.blogspot.com for more info - big4mill.blogspot.com.

Kazi zetu ni...

Tunaelimisha, kuburudisha na kadhalka.

Pata habari mbalimbali

Ndani na nje ya Tanzania/ kitaifa na Kimataifa - big4mill.blogspot.com.

Monday, 8 July 2013

QUEEN DARLEEN: KWENYE MAPENZI UBABE NAUWEKA PEMBENI

Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’.

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’ amesema pamoja na…

NEW AUDIO: WYNEM - "MWANAMBUZI"

Msanii anayekuja kwa kasi katika muziki wa Bongo Flava hapa nchini Tanzania, ambae pia amaeshafanya colabo na wasanii wakali katika gemu akiwemo Linex, Suma Mnazareth, Nick Maujanja na wengineo muite Wynem jina halisi anaitwa Mahamud Issa. Gemu la muziki wa kizazi…

Thursday, 4 July 2013

FBI wakagua ofisi ya Kova kwa mbwa


 

. Ofisa mmoja wa Usalama wa Marekani (FBI), akiwa na mbwa jana aliingia Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kufanya ukaguzi.
Tukio hilo lilitokea muda mfupi kabla ya msafara wa magari ya Marekani kupita yakitokea Ikulu kwenda Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kumlaki Rais Barack Obama.
Polisi ambaye hakutaka kutajwa alisema ofisa huyo  aliingia na mbwa hadi maeneo ya mapokezi, lakini muda mfupi walitoka.
“Walikwenda moja kwa moja mapokezi wakafanya ukaguzi,  kisha wakatoka nje ya jengo na kama hiyo haitoshi, ofisa huyo akiwa na mbwa alikwenda sehemu ya kuegesha magari yenye kesi na yale ya kawaida na kuanza kufanya ukaguzi, baada ya hapo waliondoka,” alisema polisi huyo na kuongeza:
“Licha ya mimi kutokuwa na  cheo pale, lakini hili la kutukagua na mbwa, ni kama wametudhalilisha... sisi ndiyo tunaaminika kwa usalama, leo hii wanatukagua na mbwa. Tena Kituo Kikuu.”
Hata hivyo, usalama kwenye vituo vingi ikiwamo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juliusu Nyerere, vilikuwa chini ya usimamizi na uangalizi wa makachero wa Marekani.

My Blog List